January 16, 2010

TAARIFA YA MSIBA WA MACHALO MAJIGE FAUSTIN, AU (SAMSON MUKANDYA)

MAREHEMU MACHALO MAJIGE FAUSTIN

TAARIFA YA MSIBA WA MACHALO MAJIGE FAUSTIN, AU (SAMSON MUKANDYA)
Familia ya Marehemu, Bw & Bibi, Aloycius Chokara, wa Sinza Mori Dar-es-salaam
.
Inasikitika kutangaza kifo cha Mtoto wao mpendwa MACHALO MAJIGE FAUSTIN, AU (SAMSON MUKANDYA) kilichotokea tarehe 14, 01, 2010, katika hospitali ya Muhimbili Dar-es-salaam, msiba upo nyumbani kwao Sinza Mori, Mazishi yatafanyika Tarehe 16, 01, 2010, katika makaburi ya Sinza. Saa sita kamili kutakuwa na ibada katika Kanisa Katoliki la (Mt Maxcimilian Kolbe Mwenge)
Baada ya ibada, mwili wa marehemu utapelekwa nyumbani kwao Sinza mori.
Saa nane kamili, ndugu jamaa na marafiki watatoa heshima za mwisho kwa marehemu, na baada ya heshima za mwisho, safari ya kuelekea makaburini itaanza. Watu wote mnaomfahamu MACHALO, karibuni sana ili tumsindikize
ndugu yetu na rafiki yetu, katika safari yake ya mwisho hapa duniani.
Kwa taarifa zaidi unaweza kupiga simu namba hizi,
0713652020, Joseph,
0713472930, Mang´enya,
0713131910, Samora.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe,
apumzike kwa amani amen.

No comments:

 Wale wajanja wote tunakutana Leverkusen 24.09.22