Betreff: Wabunge wa Chadema Waangwa rasmi kwa kuangalia mechi ya kimataifa
Baaada ya kazi kubwa ya kuzindua na kuimarisha tawi la chadema Washington Dc Maryland na Virginia,Wabunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)Mhe. Peter Msigwa na Mhe. Nassari Joshua, Al-Marufu Dogo janja, Usiku wa Jana Jumatano Mei 30,2011 waagwa rasmi kwa kuangalia mpambano wa kimataifa kati ya US na Brazil ndani ya uwanja wa Fedex, uliopo Landover Maryland Nchini marekani
Wabunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe, Peter Msigwa na Mhe. Nassari Joshua, Al-Marufu Dogo janja, wakiwa na uwongozi wa tawi la Chadema Washington Dc Libe Mwangombe, wanne, Mjomba a.k.a Cosmas, Mzee wa swahilivilla Aboh Shatry wa pili kulia, pamoja na mashabiki wa US, wakiiunga mkono bendera ya taifa. (Picha maelezo na swahilivilla.blog spot.com)
Idadi ya wapenzi waliohudhuria katika mpambano huo ni 67,656 wakiwemo Mhe. Nassari Joshua pamoja na Mhe, Peter Msigwa. (Picha maelezo na swahilivilla.blog spot.com)
Wabunge wa chama cha Chadema wakipata flash ya pamoja na warembo wa Kibrazil ndani ya uwanja wa FedexField, uliopo Landover Maryland Nchini marekani. (Picha maelezo na swahilivilla.blog spot.com)
Picha ya pamoja na viongozi wa juu wa Chadema kwenye mpambano wa US na Brazil Usiku wa kuamkia leo Alhamis Mei 31,2012 ndani ya ndani ya uwanja wa Fedex, uliopo Landover Maryland Nchini marekani
Nabendera ya Taifa wakishangilia Bao la kwanza la Brazil lilifungwa kwa Penalti na mchezaji Neymar
Wachezaji wa Brazil wakilinda ngome yao kwa kuwadhibiti timu ya US kwenye mechi hiyo ya kirafiki ambapo timu ya Brazil waliweza kuwabamiza US bao 4-1 nyumbani kwa
US. hoi kwa Brazil baada ya kubamizwa bao nne bao la kwanza lilifungwa na Neymar, na lapili na Thiago mnamo wa dakika ya 11, kipindi cha kwanza. bao la US lilifungwa na Hercules Gomes dakika ya 44 kipindi chakwanza hadi mapumziko Brazil 2 US 1 kwenye mchezo wa kirafiki. (Picha maelezo na swahilivilla.blog spot.com)
Malumbo´s Junior
MANENO MACHAFU NA KASHFA HAZINA NAFASI KATIKA KIWANJA HIKI. TUNAKARIBISHA MAONI YENYE KUJENGA NA KUELIMISHA JAMII.
May 31, 2012
May 30, 2012
WABUNGE PAMOJA NA VIONGOZI WA TAWI LA CHADEMA WASHINGTON DC WATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI MAREKANI
Baada ya kazi pevu ya uzinduzi wa tawi la Chadema jijini Washington Dc wabunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamtembelea rasmi Balozi wa Tanzania nchini Marekani.
Balozi wa Tanzania Nchini Marekani na Mexico Mhe. Mwanaidi Sinare Maajar akipata picha ya pamoja na Mbunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe. Peter Msigwa ndani ya Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani.
Wabunge wa Chadema Mhe. Peter Msigwa wapili kushoto, Mhe. Nassari Joshua, Al-Marufu Dogo Janja, (Watatu kulia), ofisa wa ubalozi Mhe. Peter Msigwa, Kaimu Balozi Mhe Lilian Munanka pamoja na viongozi wa tawi la Chadema Washington Dc wakipata picha ya pamoja na balozi Mhe. Mwanaidi Sinare Maajar baada ya kumtembelea rasmi siku ya Jumanne Mei 29,2012 Washington Dc Nchini Marekani.
Mbunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe. Peter Peter Msigwa akipata picha ya pamoja na waTanzania waishio nchini Marekani, ndani ya Ubalozi wa Tanzania Washington Dc. (Picha na swahilivilla.blogspot.com)
* Media Briefing note for the Global 2013 Smart Partnership Dialogue to be held in DAR ES SALAAM, TANZANIA – 24TH TO 28TH MAY, 2013
Tanzania will host the next Smart Partnership Dialogue that is scheduled to take place from 24th to 28th May, 2013 in Dar es Salaam. President Jakaya Mrisho Kikwete, is expected to officiate the National launch at noon today Tuesday May 29, 2012 at the Karimjee Hall grounds in Dar es salaam. President Kikwete had agreed to host the event during the last dialogue that took place in Putrajaya, Malaysia in June, 2011 - branded the Langkawi International Dialogue.
The Smart Partnership Dialogues are a brainchild of the Commonwealth Partnership for Technology Management. The CPTM which is the social and scientific interlinkage arm of the Commonwealth, has since 1995 undertaken in collaboration with willing national partners to provide a forum that cuts across the east-west, have, have not’s and the developed and developing dichotomy for the discussion of topical subjects in a conducive inclusive, open dialogue. Inspired by the increasing need to ensure a win-win interrelationship between actors, the CPTM, in collaboration with the host country undertake to provide an ambient setting where individuals from all walks of life and professions can meet and hold serious discourse on selected subjects every two years.
To ensure that these dialogues are successful, a two pronged approach is utilized. The first is when the host country convenes a National Dialogue. This involves the gathering together of different sectors of the host community and coming up with a topical issue that is not just locally relevant, but which resonates internationally and merits a grander discourse and focus. The second is when the Host country in collaboration with the CPTM plan for, invite participants and hold an international open dialogue on the selected topic, in essence, host a SMART DIALOGUE. As hosts, the kicking off of the National Dialogue is very crucial.
It is a means for creating National and International awareness of the next host of the Dialogue and avails the opportunity to announce the dialogue venue, topic and dates. The Launch of the National Campaign for the Dialogue in Tanzania will take place on the 29th May, 2012 at the Karimjee Hall Grounds from 10:00 am to 11:00 am. The Host and Patron Advisor for the 2013
Smart Partnership Dialogue, H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania will officially launch preparations for the 2013 Dialogue and introduce the Theme for the Dialogue (Leveraging Technology for Africa’s Socio-Economic Transformation) announce the date for the Dialogue (24th to 28th May, 2013) and the venue (Dar es Salaam) issue a holistic invitation to both the citizens of Tanzania as well as the International Community at large, and share his vision for the Dialogue.
The Dialogue has been branded the GLOBAL 2013 SMART PARTNERSHIP DIALOGUE in anticipation of interest the chosen theme is likely to raise. Technology is a global phenomenon, a global concern, a global topical issue. It is therefore more than likely that a Dialogue on Technology for development shall merit global attention and have a global audience/participation. The Execution of the preparation will be undertaken under the guidance of the Chief Secretary who is the Convener of the Dialogue.
The Chief Secretary will be supported by a National Steering Committee that comprises of Permanent Secretaries from All Ministries as well as Representatives of Keyline Sectors both on Mainland Tanzania and Zanzibar. A Focal Point Team from the Ministry of Foreign Affairs will spearhead the logistical and liaising activities necessary for the successful execution of the Dialogue. The Team will over time incorporate Members from different Links A Resource Group with an Advisory role comprising of key members of the Academia, Business and Corporate Community, Youth, Labour, Culture, Industry and Media has been set up under the leadership of Professor Samuel Wangwe.
Following the National Launch, the next step is scheduled to be contact with different Links within Tanzania who will in turn be linked with counterparts interested in participating in the Dialogue in 2013. A National Dialogue to discuss the theme will follow thereafter. Other African countries that have hosted the Smart Partnership Dialogues include Botswana, Namibia, Zambia, Zimbabwe, Mozambique, Swaziland, Lesotho and Uganda that has hosted it twice. Other countries include Barbados, and Malaysis that has hosted the dialogue nine times.
Issued by
THE FOCAL POINT TEAM, GLOBAL 2013 SMART PARTNERSHIP DIALOGUE, MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION
May 28, 2012
Uzinduzi rasmi watawi la Chadema Washington Dc na viongozi wa juu wa chadema
Uongozi wa juu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika uzinduzi rasmi watawi la Chadema Washington Dc kwenye meza ya juu wa kwanza kushoto Libe Mwangombe, akifatiwa na Mhe. Peter Msigwa, Mwenyekiti wa tawi Mhe. Kalley Pandukizi, Mhe. Zitto Kabwe, na Mhe. Nassari Joshua, Dogo Janja, mkutano huo ulifanyika kwenye ukumbi wa Mirage Hall uliopo University Of Bld, Hysattsville, Maryland Nchini Marekani
Mhe. Zitto Kabwe akitoa hutba kuelezea mpango mzima wa mambo yanavyoendelea nchini Tanzania
Kwa Audio na Video swahilivilla.blogspot.com
Mhe. Leticia Nyerere
Mhe. Maryam Msabaha
Baadhi ya wakereketwa wachukua kadi baada ya uzinduzi wa tawi la chadema WashingtonMhe. Zitto Kabwe akitoa hutba kuelezea mpango mzima wa mambo yanavyoendelea nchini Tanzania
Kwa Audio na Video swahilivilla.blogspot.com
May 22, 2012
MSONDO KUTOA BURUDANI KATIKA UKUMBI WA EMIRATE MASDASI JUNE 2


Na Mwandishi Wetu
BENDI Kongwe ya Msondo ngoma ya jijini Dar es salaam inatalajia
kufanya uzinduzi wa ukumbi mpya kabisa wa kisasa wa burudani wa
Emirate Hall uliopo Masasi June 2 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari Msemaji wa bendi hiyo Rajabu
Mhamila 'Super D' Alisema wamealikwa kwa ajili ya kutoa burudani siku
ya ufunguzi wa ukumbi huo ambapo watatoa burudani isiyo na kifani
;unajua sisi ni baba ya Muziki nchini ndio mana wapenzi wengi
wanaitaji burudani kutoka kwetu ndio mana tunapopata nafasi ya kwenda
mikoani tunakwenda kama hivi tumealikwa kutoa burudani siku hiyo
tutatoa burudani ya uhakikasiku hiyo tutapiga vibao vetu vya zamani na vipya kwa sasa alivitaja
baadhi ya vibao vitakavyonogesha uzinduzi huo kuwa ni Suluhu wa
Shabani Dede, Nadhiri ya Mapenzi wa Juma Katundu na Baba Kibene wa
Eddo Sanga hizo ni baadhi ya nyimbo mpya zitakazonogesha siku hiyo
vile vile watapiga nyimbo zao za zamani
zilizotamba wakati huo Alisema Super D Kundi hilo litaambatana na
wanamziki wake wote wakiwemo wakongwe katika mziki wa Dansi Nchini
Maalimu Gulumo ' Kamana' Saidi Mabela ' DKT Mabela' na wengine wote
watafanya vitu vyao siku hiyo kwa ajili ya kukonga nyoyo za mashabiki
wao wa Masasi Aliongeza Super D
April 24, 2012
FRANCIS CHEKA NA JAPHET KASEBA KUPAMBANA TENA SIKU YA SABA SABA
Japhetá Kaseba amesaini mkataba
Na Mwandishi Wetu
BINGWA wa kick Boxing. Japhetá Kaseba amesaini mkataba wa kucheza na
Bingwa wa dunia wa ndondi mkanda unaomilikiwa na IBC, Francis Cheka wa Morogoroá katika uzani wa KG 75 utakaofanyika siku ya sabasaba jijini Dar es Salaam
Akizungumza wakati wa kusaini mkataba huo Kaseba amesema anashukulu kupata mpambano huo na atahakikisha anaonesha uwezo wake wote katika mchezo huo kwani yeye ni bingwa wa mapambano
Najua mabondia wa hapa bongo wananikwepa sana kwa kuwa nimeshakuwa bingwa wa ngumi za mateke lakini awajui mimi ni bingwa katika mapigano yote alisema Kaseba;
Nitahakikisha naweka kambi ya kutosha na kukata ngebe za cheka ni mtoto mdogo sana katika masumbwi kwa kweli bingwa wa kweli ni Rashidi Matumla ambaye ninamuheshimu mpaka sasa cheka kanikimbia mda mrefu tu tangia tupambane 3 October 2009á ambapo alipewa ubingwa kwa kusingizia mshabiki wangu alikuja kumtupa nje ya uwanja kazi yake yeye anarudiana na Mada Maugo kila siku lakini kwa sasa kakanyaga miwaya zamu yake imefika,
Nae Promota wa mpambano huo Kaike Siraju amesema mpambano huo utakaofanyika Dar es salaam siku ya sabasaba utakuwa ni mpambano ambao aujawai kutokea kwa kuwa mabondia hao wanakubalika na mashabiki wa ndani na nje ya Nchi
Mbali na mpambano huo pia kutakua na mapambano ya utangulizi na burudani mbalimbali ambazo mtatangaziwa baadae.
Na Mwandishi Wetu
BINGWA wa kick Boxing. Japhetá Kaseba amesaini mkataba wa kucheza na
Bingwa wa dunia wa ndondi mkanda unaomilikiwa na IBC, Francis Cheka wa Morogoroá katika uzani wa KG 75 utakaofanyika siku ya sabasaba jijini Dar es Salaam
Akizungumza wakati wa kusaini mkataba huo Kaseba amesema anashukulu kupata mpambano huo na atahakikisha anaonesha uwezo wake wote katika mchezo huo kwani yeye ni bingwa wa mapambano
Najua mabondia wa hapa bongo wananikwepa sana kwa kuwa nimeshakuwa bingwa wa ngumi za mateke lakini awajui mimi ni bingwa katika mapigano yote alisema Kaseba;
Nitahakikisha naweka kambi ya kutosha na kukata ngebe za cheka ni mtoto mdogo sana katika masumbwi kwa kweli bingwa wa kweli ni Rashidi Matumla ambaye ninamuheshimu mpaka sasa cheka kanikimbia mda mrefu tu tangia tupambane 3 October 2009á ambapo alipewa ubingwa kwa kusingizia mshabiki wangu alikuja kumtupa nje ya uwanja kazi yake yeye anarudiana na Mada Maugo kila siku lakini kwa sasa kakanyaga miwaya zamu yake imefika,
Nae Promota wa mpambano huo Kaike Siraju amesema mpambano huo utakaofanyika Dar es salaam siku ya sabasaba utakuwa ni mpambano ambao aujawai kutokea kwa kuwa mabondia hao wanakubalika na mashabiki wa ndani na nje ya Nchi
Mbali na mpambano huo pia kutakua na mapambano ya utangulizi na burudani mbalimbali ambazo mtatangaziwa baadae.
April 23, 2012
GARI LA CHEKA & MAUGO ILI HAPA
Msemaji wa Mpambano wa Ngumi kati ya Mada Maugo na Francis Cheka , Yasini Abdallah akionesha mkana na gari atakalopewa mshindi wa mpambano huo.
Johannes Lugenge kushoto na Promota wa Mpambano wa Mada Maugo na Francsis Cheka, Lucas Rutainurrwa wakionesha mkana wa Ubingwa wa I.B.F Afrika na gari atakalochukua bingwa wa mchezo huo Dar es salaam.Waandaaji wa pambano la ubingwa wa IBF kati ya Francis Cheka na Mada Maugo leo wameonesha rasmi gari watakalogombania Mabondia Mada Maugo Na Francis Cheka Aprili 28 mwaka huu katika ukumbi wa PTA, Dar es Salaam.
Pambano hilo linatarajiwa kuwa katika uzito wa kg 75 la raundi 12 la Kimataifa ambapo linatarajiwa kuwa chini ya Kamisheni ya Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC) huku majaji wa pambano hilo wakitegemewa kutoka nje ya nchi.
Akizungumza Dar es Salaam leo, Msemaji wa mpambano huo Yasini Abdallah alisema kuanikwa kwa mkanda huo na Gari kuwekwa Hadharani kutaashiria kupamba moto kwa pambano hilo ambalo linatarajia kuwa katika ngazi ya Kimataifa ili kuweza kupatikana kwa mshindi wa halali na pia itafuta hisia za kuwepo na ubabaishaji katika pambano hilo.
“Tunauanika Gari na mkanda ili kuwathibitishia wadau wa ngumi na mashabiki kwa ujumla kuwa tupo makini na pambano hili na sio la kibabaishaji na kama tulivyosema awali kuwa majaji watoka nje ya nchi na hiyo yote ni kutaka mchezo uchezeshwe kulingana na hadhi ya mkanda,” alisema Kaike.
Alisema, maandalizi kwa ujumla ya pambano hilo yanaendelea vizuri na zawadi ya gari kwa mshindi iko pale pale ambapo mshindi atakabidhiwa siku hio hio ya pambano baada a kutangazwa mshindi na kupewa mkanda itafuatiwa na zawadi hiyo ya gari.
Awali mabondia hao walishakutana mara mbili ulingoni ambapo katika pambano la kwanza lilofanika PTA Cheka alishinda kwa pointi ambapo Maugo hakukubali matokeo hao na kuandaliwa pambano la marudiano lilofanyika Uwanja wa Jamuhuri Morogoro ambapo Cheka aliibuka mshindi tena kwa kumtwanga kwa pointi.
Baada ya kumalizika kwa pambano hilo kila bondia aligoma kucheza na mwenzake tena lakini baada ya kuandaliwa pambano hilo la ubingwa kila mmoja alibadilisha nia na kuamua kurudi ulingoni kuwania mkanda huo.
Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD zenye mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywherth, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis na wengine kiba DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.
“Ninatarajia kuwepo kwa ajili ya kuwauzia DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika pambano la Cheka na Maugo ili kuweza kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo wa ngumi”, alisema Super D .
April 14, 2012
MSANII ALI KIBA ADAIWA KUHOJIWA NA POLISI KUHUSIANA NA MADAI KUWA NDO ALIMPATIA ELIZABETH MICHAEL 'LULU' LIFTI SIKU KANUMBA ALIYO FARIKI...!!!

Habari kutoka Mwanaspoti zinasema msanii wa muziki wa Bongo Flava, Ali Kiba, anadaiwa kuhojiwa na polisi kwa maelezo ndiye aliyempa Elizabeth Michael Lulu msaada wa usafiri (lifti) baada ya kutoka kwa Steven Kanumba.
Lulu ndiye anayetuhumiwa kuhusika na kifo cha Kanumba kilichotokea usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita.
Kachero aliyemhoji Lulu Jumatatu wiki hii, amedai kuwa msanii huyo alihojiwa katika kituo cha Polisi cha Oysterbay kutokana na kutajwa na mtuhumiwa kuwa ndiye aliyempatia lifti baada ya kutoka kwa Kanumba.
Mwanaspoti lilimtafuta Ali Kiba ili azungumzie taarifa hizo, alipopatikana kwa njia ya simu, msanii huyo alisema: "Samahani kaka siwezi kuzungumzia chochote kuhusu mambo hayo."Kisha akakata simu.
Lulu alitoa maelezo yake polisi Jumatatu ikiwa ni saa 65 tangu kutokea kwa kifo cha Kanumba., ambapo alizungumza na kachero wa Makao Makuu ya Polisi ambaye pia ana taaluma ya saikolojia.
Taarifa za uhakika ambazo Mwanaspoti limezipata kutoka ndani ya Jeshi la Polisi zinaonyesha kuwa kachero huyo (jina tunalo) aliyetoka makao makuu alifanikiwa kufanya mahojiano na binti huyo ambaye awali aligoma. Imeelezwa kuwa, alitumia takribani sasa tatu kumlainisha Lulu azungumze.
Katika mahojiano na gazeti la The Citizen Jumanne, kachero huyo ambaye alitoka katika Kitengo cha Upelelezi wa Makosa ya Jinai alisema tayari amemhoji mtuhumiwa namba moja Lulu pamoja na msanii huyo maarufu wa muziki wa kizazi kipya kufuatia kifo cha Kanumba, aliyefariki usiku wa kuamkia Jumamosi.
Akimnukuu Lulu katika mazungumzo yake, kachero huyo alisema Lulu aliitwa na marehemu Kanumba ili waweze kutoka (out) kwenda kwenye bendi ya Mashujaa ambayo ilikuwa inapiga kwenye kiwanja chao cha nyumbani, Vingunguti. Mtuhumiwa alionekana kutokuwa tayari, lakini marehemu akamlazimisha Kachero huyo alisema: Lulu anadai alifika nyumbani kwa marehemu saa tano usiku, lakini akiwa ameweka msimamo wa kutokwenda sehemu yoyote usiku ule, lakini Kanumba alikuwa akilazimisha ndipo yakatokea mabishano na marehemu akafunga mlango kwa funguo.
"Hata hivyo, baada ya ugomvi wa kama nusu saa hivi, Lulu alifanikiwa kuondoka chumbani humo na alifungua mlango kwa taharuki na kuondoka bila kujua kilichotokea nyuma, huku akimweleza ndugu wa marehemu kwamba Kanumba ameanguka."
Mpashaji habari wetu huyo alisema, kumekuwa na jumbe fupi za maneno kutoka kwa wanasiasa ambazo zimekuwa zinaingia kwenye simu ya kiganjani ya Lulu, zikiahidi kumsaidia.
Alionya kuwa kama wanasiasa wataanza kuingilia uchunguzi wa Polisi katika kesi hiyo ambayo imevuta hisia za watu wengi, wanaweza kuharibu mambo. Lakini yeye mwenyewe akionyesha kwamba yuko imara na anafahamu anachokifanya.
Kuhusu msanii wa muziki wa kizazi kipya, Ali Kiba, kachero huyo alisema kwamba alihojiwa kutokana na kutajwa na mtuhumiwa kama mtu aliyempatia msaada wa usafiri (lifti) baada ya kutoka kwa Kanumba.
Kachero huyo alisema kutokana na taarifa ambazo wanaendelea kuzipata, kuna uwezekano watu wengi zaidi wakahojiwa ili kujiridhisha kabla ya watuhumiwa kuanza kupandishwa kizimbani baada ya upelelezi kukamilika.Lulu alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jumatano wiki hii na kutotakiwa kujibu chochote kwa vile mahakama hiyo haina uwezo wa kisheria wa kusikiliza kesi za mauaji.
April 13, 2012
April 07, 2012
Msanii Nyota Steven Kanumba Afariki Dunia

STEVEN KANUMBA WAKATI WA UHAI WAKE
KWA MUJIBU WA MDOGO WA MAREHEMU STEVE KANUMBA, ALISEMA KUWA ELIZABETH MICHAEL MAARUFU KAMA LULU ALIKUJA NYUMBANI KUKAWA NA KAUGOMVI AMBAPO WAKAINGIA CHUMBANI WAKIWA HUKO BAADA YA MUDA,LULU ALITOKA NA KUMUITA YEYE KUMUAMBIA KANUMBA KAANGUKA, YE ALIPOENDA AKAMKUTA KAANGUKA NDIO AKAENDA MUITA DAKTARI WA KANUMBA AMBAPO ALIPORUDI HAKUMKUTA LULU, LAKINI HADI TUNAVYOONGEA LULU YUKO POLISI OSTERBAY KWA AJILI YA MAHOJIANO NA POLISI, NA MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA MUCHUARI MUHIMBILI.
Subscribe to:
Posts (Atom)
