October 05, 2019

Watanzania wa Ujerumani wafanya Uchaguzi

Umoja wa Watanzania Ujerumani UTU e.V umefanya mkutano mkuu wa kuchagua viongozi mjini Aschaffenburg nchini Ujerumani siku ya jumamosi tarehe 28.09.2019.
Katika uchaguzi huo watanzania wanaoishi nchini ujerumani walichagua viongozi wapya , nafasi ya M/kiti  alichaguliwa Bi Vanessa Fölsen kuchukua nafasi M/kiti Mstaafu Bwana Mfundo Peter Mfundo aliyejiuzulu nafasi hiyo baada ya kuitumikia takribani miaka 9. hata hivyo kamati ilimpendekeza Bwana Mfundo achukue nafasi ya heshima kuwa mwanakamti , mshauri na mlezi wa UTU e.V na kiongozi  muandamizi katika shughuli za UTU e.V
Watanzania wanaoishi ujerumani pia walichagua viongozi wafuatao
M/kiti:  Bi.Vanessa Fölsen
Makamu M/kiti: Bw. Malumbo Salim Malumbo
Katibu: Bi Petrida Karch
Mtunza Pesa:Bw.Mngoya Lukuta

wanakamati waliochaguliwa

Bw. Mfundo Peter Mfundo
Bw.Ebrahim Makunja (aka. Kamanda Ras Makunja )
Bw. Sudi Mnette

No comments:

 Wale wajanja wote tunakutana Leverkusen 24.09.22