May 01, 2008

Ndoto ya bayern yaishia njiani

Oliver Kahn

Timu ya bayern munich ambayo inatazamiwa kuwa mabingwa wa ujerumani mwaka huu imeyaaga mashindano ya UEFA kwa kufungwa mabao 4-0 bila huruma na timu ya Zenit kutoka St. Petersburg/Urusi. hiyo ilikuwa mechi muhimu sana kwa kipa wao Olli kahn ambaye anamaliza muda wake mwaka huu. Olli alitegemea kumaliza wakati wake kwa kuchukua vikombe vitatu lakini kwa bahati mbaya Zenit imeikatisha ndoto hiyo katikati. kwahiyo Olli atawaaga wapenzi wa kabumbu wa ujerumani kwa vikombe 2 ambavyo kimoja cha chama cha mpira ujerumani la wamekwishachukua na sasa wako njiani kuchukua cha ubingwa wa kabumbu ujerumani.

No comments:

 Wale wajanja wote tunakutana Leverkusen 24.09.22