May 05, 2009

MISS TANZANIA EU YAPAMBA MOTO


Katika kuhakikisha burudani, ubunifu  , sanaa na utamaduni kitanzania unawakilishwa ipasavyo katika shindano la urembo,; Miss Tanzania EU 09 litakalo fanyika mjini Essen Germany, wasanii mbali mbali kutoka bongo wamealikwa...
Akielezea Blog ya jamii  mratibu wa mashindano hayo Nashe Mvungi amesema  wasanii wa muziki wa kizazi kipya MB Dogg  na Bushoke watapanda jukwaani kutumbuiza, mbali na hao kutakua na makundi mengine ya burudani kutoka sehemu mbalimbali za Ulaya.

Katika kinyangányiro hicho mgeni wa heshima ni Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mheshimiwa A.Ngemera.
Akizungumzia washiriki wa mashindano hayo Nashe alisema nafasi bado ziko wazi kwa watakaotaka kushiriki, form za kushiriki  zipatikana katika www.misstanzania.eu  au email info@misstanzania.eu

Vile vile mratibu huyo alisisitiza kuwa washindi wa 3 wa mwanzo  watapata nafasi ya kwenda United Kingdom kwenye mpambano wa Miss Tanzania mjini London.

No comments:

 Wale wajanja wote tunakutana Leverkusen 24.09.22